Abstract

Lengo la makala hii ni kujadili fursa na changamoto kwa maendeleo endelevu ya lugha ya Kiswahili, hususan baada ya Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni - UNESCO kutangaza Siku ya Maalumu ya Kiswahili duniani. Kutangazwa kwa siku hii kunatoa fursa kwa wadau wa Kiswahili katika ngazi zote za kitaifa na kimataifa kujadili masuala mbalimbali yanayohusiana na maendeleo ya Kiswahili. Katika makala hii, pamoja na masuala yaliyolengwa, mwandishi anatoa shukurani zake kwa asasi mbalimbali za kimataifa ambazo zimeshiriki kwa namna tofauti katika mchakato wa kufanikisha hatua ya kutangazwa tarehe 7 Julai kuwa siku maalumu ya Kiswahili duniani. Makala hii inajadili kwa ujumla, majukumu na mchango wa wadau mbalimbali katika maendeleo ya Kiswahili kwa kudokeza fursa na changamoto katika maendeleo hayo. Mtafiti anahitimisha kwa kusisitiza kuwa jukumu la kuendeleza lugha ni la taasisi zote za elimu, hususan vyuo vikuu vya ndani na nje ya nchi. Kutokana na changamoto kubwa ya kifedha, uzalendo uwekwe mbele ili kufanikisha malengo ya kukuza Kiswahili.

Full Text
Paper version not known

Talk to us

Join us for a 30 min session where you can share your feedback and ask us any queries you have

Schedule a call

Disclaimer: All third-party content on this website/platform is and will remain the property of their respective owners and is provided on "as is" basis without any warranties, express or implied. Use of third-party content does not indicate any affiliation, sponsorship with or endorsement by them. Any references to third-party content is to identify the corresponding services and shall be considered fair use under The CopyrightLaw.